Sunday, 7 October 2012

EL CLASICO: Nou Camp, BARCA v REAL!

Posted at  02:11  |  in  

BARCA_v_REALNI El Clasico, Bigi Mechi, lakini kwa Mabingwa watetezi Real Madrid ushindi ni lazima kwa vile tu, baada ya Mechi 6 za La Liga, wapo Pointi 8 nyuma ya vinara Barcelona ambao wameshinda Mechi zao zote 6 za Ligi Msimu huu.
Chini ya Meneja Tito Vilanova, aliembadili Pep Guardiola, Barcelona wana Pointi 18 na wamefunga bao 17 na kufungwa 5 tu kwenye Mechi zao 6 za Ligi.
Licha ya kushinda Supercopa mwanzoni mwa Msimu baada ya kuifunga Barca bao 2-1 katika Mechi ya pili baada ya kuipoteza ya kwanza kwa 3-2 huko Nou Camp, Mabingwa Real Madrid, chini ya Kocha machachari Jose Mourinho, wamejikuta wakianza kampeni yao ya kutetea Taji lao la Liga kwa kulegalega kufuatia kufungwa na Sevilla na Getafe, na sare na Valencia, na kuwaacha Wadau wao wakitoa sababu
kibao za kudorora huko.
Wengine wanadai ‘kutokuwa na furaha’ kwa Nyota wao Cristiano Ronaldo kumechangia, wengine wanasema ‘bifu’ la Mourinho na Zinedine Zidane aliekuwa Mkurugenzi wa Ufundi kumechangia huku kukiwa na ‘bifu’ jingine kati ya Mourinho na Sergio Ramos.
Lakini, kwa lolote lile, Real Madrid wanahitaji ushindi kwenye El Clasico hii au watajikuta wako Pointi 11 nyuma ya Barcelona.
Zipo dalili njema kwao kwa Timu yao kuanza kubadilika hivi sasa huku Ronaldo akipiga hetitriki mbili mfululizo, ile ya kwenye ushindi wa 5-1 dhidi ya Deportivo La Coruna na ile ya juzi kwenye UEFA CHAMPIONZ LIGI walipoichapa Ajax huko Amsterdam bao 4-1.
Lakini Barcelona wakishinda Mechi hii ya Jumapili litakuwa pigo kubwa kwa Real ambao watakuwa Pointi 11 nyuma.

Share this post

Kuhusu Mdaku Orijino

Tunafichua maovu, uozo na taka taka zoote wanazofanya watu wasio na staha. Unapicha yoyote habari yoyote ya washenzi wa tabia, tucheki tuwaanikeGoogle+.

0 comments:

About-Privacy Policy-Contact us
Copyright © 2013 BONGO MAGAZINE 1. by Mdakuzi
Proudly Powered by Blogger.
back to top