Sunday 30 September 2012

MJI WA AJABU 'ORDOS' THE GOST CITY OF CHINA

Posted at  05:12  |  in  

  MJI WA AJABU 'ORDOS' THE GOST CITY OF CHINA

Hizi  ndo picha za  mji wa ORDOS uliopo China, mji huu umekua mji wa maajabu na umebatizwa jina la 'GHOST CITY'.
Baadhi ya mitaa ikiwa tupu katika mji huo
Mji huu ni mji wa pili kwa ubora wa miundombinu na majengo baada ya ule mji wa Beijing na ulijengwa kwa muda wa mwaka mmoja tu, mji huu ulijengwa mwaka 20... baada ya mtikisiko wa kiuchumi ulipoikumba dunia kiujumla, Serikali ya China iliamua kuujenga mji huu ili kuyanusuru makampuni ya ujenzi ya chini kutokana na mtikisiko wa Uchumi uliokuwepo kipindi hicho kwa kuyapa tenda ya kuujenga mpaka kukamilika. Tazama Picha zake Hapa, hizi ni baadhi tu ya picha zipo nyingine nyingi zaidi..
Nyumba nyingi hizi zote hazina wakaaji

Baadhi ya Majengo yaliyopo katika mji wa Ordos

Mitaa ikiwa tupu bila watu

Kitu cha ajabu ambacho kinafanya huu mji uitwe Ghost City ni ile hali yake ya kutokuwa na wakaazi, Mji una kila kitu lakini idadi ya watu wanaoishi katika mji huo ni ndogo sana, na hii inatokana na ukali wa maisha katika mji huo, watu wengi wamepanga nyumba katika mji huo lakini hawajaanza kuishi huko kwa kukwepa gharama kubwa za maisha..........Tanzania ina mpango wa kujenga mji mpya wa kigamboni kuanzia 2011-2030, hebu linganisha na wenzetu....wao wamejenga huo mji ambao ni mkubwa sana zaidi ya miji mingine huko china kwa mwaka mmoja.....sie KIGAMBONI itachukua miaka 20!! Speed yetu inaridhisha kweli???????? Na je, KIGAMBONI nayo haitageuka kuwa GHOST CITY???? Maoni yako please

Share this post

Kuhusu Mdaku Orijino

Tunafichua maovu, uozo na taka taka zoote wanazofanya watu wasio na staha. Unapicha yoyote habari yoyote ya washenzi wa tabia, tucheki tuwaanikeGoogle+.

0 comments:

About-Privacy Policy-Contact us
Copyright © 2013 BONGO MAGAZINE 1. by Mdakuzi
Proudly Powered by Blogger.
back to top