Saturday, 22 September 2012

Ligi kuu England kesho hapatoshi ni Liverpool v Man United

Posted at  09:32  |  in  

Kesho ni patashika nguo kuchanika,ni usemi maarufu inapotokea kuwa na mechio kali au jambo kubwa. Kwa wale wapenzi wa soka kesho liverpool and Manchester united watavaana kuwania pointi tatu muhimu katika uwanja wa Anfield mida ya saa tisa na nusu kwa masaa ya Africa mashariki, wakati huohuo Zipo taarifa za kuaminika ndani ya Liverpool na Manchester United kuwa Wachezaji Luis Suarez na Patrice Evra watapeana mikono kabla ya Mechi kati ya Timu hizo  katika mpambano wa Ligi Kuu England.
Huku Mechi hiyo ikigubikwa na kumbukumbu ya maafa yaliyotokea Mwaka 1989 wakati Mashabiki 96 wa Liverpool walipofariki Uwanjani Hillsborough kwenye Mechi ya Nusu Fainali ya FA Cup kati ya Liverpool na Nottingham Forest baada ya msongamano na mkanyagano na Ripoti yake ya Uchunguzi kutolewa hivi juzi, Maafisa wa Klabu hizi kubwa huko Uingereza ambazo zina uhasama wa jadi wamekutana ili kupoza mlipuko wowote kwenye Mechi hiyo na hasa kutaka kuufuta uhasama kati ya Wachezaji hao wawili baada ya Suarez kufungiwa kufuatia kumkashifu kibaguzi Evra Msimu uliopita kwa kuwataka wapeana mikono.
Katika Mechi ya mwisho walipokutana, Suarez aligoma kupokea mkono wa Evra.
Tayari Meneja wa Manchester United, Sir Alex Ferguson, ameshatamka kuisapoti Liverpool katika wakati wao mgumu na Klabu hizi zimepanga kuikumbuka Siku hiyo ya Maafa ya Hillsborough kwa Manahodha Steven Gerrard wa Liverpool na Nemanja Vidic wa Manchester United kurusha Maputo 96 kabla Mechi kuanza ikiwa ishara ya kumbukumbu.
Pia Majukwaa ya Mashabiki yatapambwa na Mabango ya Halaiki huku Jukwaa moja likiandika ‘Ukweli’, jingine likitoa ishara ‘Haki’ na la tatu likisema ’96.’
Kuhusu hilo, Ferguson ametamka: “Itakuwa Siku ya kumbukumbu nzito. Tutawasapoti Liverpool kwa kila njia tunayoweza.”

Share this post

Kuhusu Mdaku Orijino

Tunafichua maovu, uozo na taka taka zoote wanazofanya watu wasio na staha. Unapicha yoyote habari yoyote ya washenzi wa tabia, tucheki tuwaanikeGoogle+.

0 comments:

About-Privacy Policy-Contact us
Copyright © 2013 BONGO MAGAZINE 1. by Mdakuzi
Proudly Powered by Blogger.
back to top