Kwa mara ya kwanza tangu 1989, Tottenham
wamefanikiwa kuifunga Manchester United bao 3-2 katika Mechi ya Ligi
Kuu England iliyochezwa Old Trafford.Kocha huyo mzoefu wa ligi kuu england amesema timu yake haikua na bahati katika mchezo huo baada ya kosakosa nyingi.
Spurs walitangulia kupata bao mbili kwa
kuisambaratisha Difensi ya Man United kwa kutumia kasi iliyoonyesha
uzito wa Difensi hiyo kwa bao za Fulbeki Jan Vertonghen na ‘mkimbiaji’
Gareth Bale.
Bao hizo 2-0 zilidumu hadi mapumziko.
Kipindi cha Pili Man United walibadilika
na kuonyesha wazi wazi hawakustahili kufungwa Mechi hii pale
alipoingizwa Wayne Rooney na kumtengenezea Nani kufunga bao la kwanza
lakini hapo hapo Spurs, wakidhirisha udhaifu wa Difensi ya Man United,
wakapiga bao la tatu kupitia Clint Dempsey.
Shinji Kagawa aliifungia Man United bao
la pili na waliendelea kutawala lakini walishindwa kupata bao la
kusawazisha licha ya kosa kosa nyingi.
VIKOSI:
Manchester United: Lindegaard; Rafael, Ferdinand, Evans, Evra; Carrick, Scholes; Nani, Kagawa, Giggs; Van Persie.
Akiba: De Gea, Wootton, Anderson, Cleverley, Hernandez, Rooney, Welbeck.
Tottenham Hotspur: Friedel; Walker, Gallas, Caulker, Vertonghen; Sandro, Dembele; Lennon, Dempsey, Bale; Defoe.
0 comments: