Wednesday 24 October 2012

Philipo Mulugo: Awakilisha umburura wa viongozi watanzania

Posted at  08:19  |  in  siasa




 
 
 Naibu Waziri Wa Elimu Na Mafunzo Ya Ufundi nchini Tanzania Mh. Philipo Augustino Mulugo, ameonyesha ukilaza na umbumbumbu wa hali ya juu wakati akiwasilisha mada katika Mkutano wa Elimu na Ugunduzi kwa nchi za Kiafrika.

Mkutano huo uliofanyika kuanzia tarehe 5 mpaka 7 mwezi Oktoba 2012 jijini Cape Town nchini Africa, uliwakusanyisha wataalamu mbalimbali wa elimu na ufundi kutoka nchi za Kiafrika.

Tanzania ambayo kwenye mkutano huo mada yake iliwasilishwa na Mbunge wa jimbo la Songwe ambaye pia ni Naibu Waziri Wa Elimu Na Mafunzo Ya Ufundi Mh. Philipo Mulugo. Mada zote kwenye mkutano huo zilitakiwa kuwasilishwa katika lugha ya Kingereza huku ikionekana dhahiri kabisa juu ya uwezo mdogo katika uzungumzaji na usomaji wa lugha hiyo kwa waziri huyo.

Naibu Waziri huyo ambaye alianza kujiumauma katika utambulishi wa mada yake, aliboronga zaidi pale alisema kuwa Tanzania iliundwa baada ya kuziunganisha nchi za Tanganyika na visiwa vya Zimbabwe na Pemba.

Ilitegemewa kwa mtu yeyote ambaye amefanya kosa kama hilo ni kuweza kujisasahisha kwa haraka na kuwapa maelezo sahihi wajumbe katika mkutano huo lakini haikuwa hivyo kwa Naibu Waziri huyo, kwani alionyesha ukilaza na umbumbumbu wa hali ya juu kwa kuendelea na utoaji mada katika mkutano huo.

Kitendo hicho ambacho kimewakasirisha na kuwatia aibu Watanzania wengi hususani wale ambao ni watumiaji wa mitandao ya kijamii na blogu mbalimbali. Watanzania wengi wamehoji ni kwa nini Naibu Waziri huyo ambaye ameonyesha ana uwezo mdogo sana katika uwasilishaji mada atawezaje kuhimili na kuwa dira na chachu katika maendeleo ya elimu nchini Tanzania, je mtu kama huyu ni wa kutegemewa kuinua na kuleta mapinduzi katika elimu.

Wakati umefika kwa Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania kuteuwa viongozi ambao wana uwezo wa hali ya juu katika uendeshaji wa wizara mbalimbali.

Unaweza kuangalia video ya Mh. Philipo Mulugo wakati akiwasilisha mada hiyo katika hii blog.

Share this post

Kuhusu Mdaku Orijino

Tunafichua maovu, uozo na taka taka zoote wanazofanya watu wasio na staha. Unapicha yoyote habari yoyote ya washenzi wa tabia, tucheki tuwaanikeGoogle+.

0 comments:

About-Privacy Policy-Contact us
Copyright © 2013 BONGO MAGAZINE 1. by Mdakuzi
Proudly Powered by Blogger.
back to top